Monday, September 21, 2015

CHUO CHA SANAA BAGAMOYO KUFANYA TAMASHA LA 34.



          Taasisi ya sanaa na utamaduni bagamoyo inatarajia kufanya Tamasha kubwa ambalo litakuwa ni Tamasha la 34 tangu taasisi hiyo kuanzishwa, tamasha ambalo litafanyika katika Kumbi na viunga vya Taasisi ya Sanaa na utamaduni Bagamoyo.  

Wanafunzi wa Chuo Cha Sanaa Bagamoyo.
          Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Mwenyekiti wa Tamasha hilo John Mponda amesema Tamasha litafanyika tarehe 21 hadi 27 na litahudhuriwa na watu kutoka nchi mbalimbali lengo na madhumuni ni kuwapa fursa wanafunzi kuonyesha kile walichojifunza kutoka chuoni hapo.
          Aidha, Mponda amesema tamasha hilo ambalo kauli mbiu yake ni SANAA NA UTAMADUNI KATIKA UCHAGUZI HURU NA AMANI, kauli mbiu ambayo inahakisi uchaguzi Mkuu hapa nchini hivyo kuwakumbusha watanzania na wao hawako nyuma kuitakia nchi amani na utulivu katika kipindi hiki cha uchaguzi.

No comments:

Post a Comment