Alikiba ni msanii mkubwa kuliko Davido na Wizkid jijini Lubumbashi,
katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, kwa mujibu wa staa wa filamu wa
nchini humo, Iqbar Mohamed Bagati.
Lubumbashi ni mji wa pili kwa ukubwa DR Congo baada ya Kinshasa.
Akiongea na Bongo5, Mohamed ambaye yupo nchini alipokuja kutengeneza connection na waigizaji wa Tanzania, amedai kuwa Alikiba anaweza kujaza uwanja wa mpira hata kwa siku tatu mfululizo kwa jinsi anavyokubalika huko.
Iqbar Mohamed Bagati.
Amesema kuwa staa huyo wa ‘Aje’ ni kipenzi cha watu wengi jijini humo hususan wanawake.
“Alikiba anamshinda Davido, Wizkid, labda tunaweza kumlinganisha na akina P-Square huko Lubumbashi,” amesema Mohamed. Davido alishawahi kutumbuiza mjini humo kwa takriban mara nne na P-Square karibu mara mbili.
“Alikiba ni maarufu sana Lubumbashi.”
Mohamed amesema kama Alikiba akiamua kwenda huko Lubumbashi atashangaa mapokezi atakayoyapata.
Lukumbashi ni jiji lililopo kwenye jimbo la Katanga na ni nyumbani kwa klabu ya TP Mazembe. Watu wengi wa jimbo hilo huongea Kiswahili vizuri.
Lubumbashi ni mji wa pili kwa ukubwa DR Congo baada ya Kinshasa.
Akiongea na Bongo5, Mohamed ambaye yupo nchini alipokuja kutengeneza connection na waigizaji wa Tanzania, amedai kuwa Alikiba anaweza kujaza uwanja wa mpira hata kwa siku tatu mfululizo kwa jinsi anavyokubalika huko.
Iqbar Mohamed Bagati.
Amesema kuwa staa huyo wa ‘Aje’ ni kipenzi cha watu wengi jijini humo hususan wanawake.
“Alikiba anamshinda Davido, Wizkid, labda tunaweza kumlinganisha na akina P-Square huko Lubumbashi,” amesema Mohamed. Davido alishawahi kutumbuiza mjini humo kwa takriban mara nne na P-Square karibu mara mbili.
“Alikiba ni maarufu sana Lubumbashi.”
Mohamed amesema kama Alikiba akiamua kwenda huko Lubumbashi atashangaa mapokezi atakayoyapata.
Lukumbashi ni jiji lililopo kwenye jimbo la Katanga na ni nyumbani kwa klabu ya TP Mazembe. Watu wengi wa jimbo hilo huongea Kiswahili vizuri.
No comments:
Post a Comment