Thursday, September 21, 2017

Bingwa wa masumbwi wa dunia, LaMotta afariki

Bingwa wa zamani wadunia wa Marekani wa uzito wa kati na mchekeshaji, Jake LaMotta amefariki dunia Septemba 19 mwaka huu akiwa na umri wa 95.



LaMotta ambaye alitamba zaidi katika tasnia ya mchezo wa ngumi kuanzia miaka ya 1949 hadi 1951 amefariki nyumbani kwake kutokana na tatizo la homa ya mapafu.

Kifo cha bingwa huyo wa uzito wa kati wa Marekani, Giacobbe LaMotta kilitangazwa kupitia  mtandao wa kijamii na mtoto wake  mkubwa wa kike ambaye bondia huyo alizaa na mke wake wa pili mwanamitindo Vikki LaMotta.

No comments:

Post a Comment