Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa
Ligi imepitia ripoti za michezo yote ya Ligi Kuu Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja Pili (SDL) na
kufanya uamuzi ufuatao.


Mechi namba 54 (Simba 4 v Njombe Mji 0).
Klabu
ya Simba imepewa Onyo Kali kutokana na Kocha wake Msaidizi Masoud Djuma
kuanza kufundisha bila kuwa na vibali vya kuishi na kufanya kazi
nchini. Uamuzi huo umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(13) ya Ligi Kuu
kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Pia
klabu hiyo imetakiwa kufikia Novemba 10 iwe imewasilisha Bodi ya Ligi
nakala ya vibali hivyo, na kukumbushwa kuwa mahitaji ya nyaraka hizo ni
kwa mujibu wa Kanuni za Ligi, lakini pia sheria za nchi.
Vilevile
klabu ya Simba imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa timu yake
kuwasilisha orodha ya wachezaji wake (team match list) nje ya muda wa
kikanuni. Kitendo cha timu hiyo ni kukiuka Kanuni ya 14(2k) ya Ligi Kuu.
Adhabu dhidi yao imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Klabu
ya Njombe Mji imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na
kuonesha vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina katika mechi hiyo
wakati ikiwasili uwanjani. Adhabu dhidi ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1)
ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 56 (Stand United 0 v Yanga 4). Klabu
ya Stand United imetozwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kutokana na
golikipa wao kuvaa jezi yenye namba tofauti na ile iliyosajiliwa,
kitendo ambacho ni ukiukaji wa Kanuni ya 60(11) ya Ligi Kuu kuhusu
Usajili. Adhabu dhidi yao imezingatia Kanuni ya 60(12) ya Ligi Kuu.
Mechi namba 57 (Azam FC 1 v Mbeya City 0). Mwamuzi
Shakaile Ole Yanga Lai amefungiwa miezi mitatu kwa kutoripoti na
kuchukua hatua dhidi ya kitendo cha Kipa Owen Chaima wa Mbeya City
kumpiga kofi mshambuliaji wa Azam FC. Kitendo cha Mwamuzi huyo ni
ukiukaji wa Kanuni ya 38(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Waamuzi
wakati adhabu dhidi yake imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 38(5) ya Ligi
Kuu.
Naye
Kamishna wa mechi hiyo, David Lugenge amefungiwa miezi mitatu kwa
kushindwa kuripoti tukio hilo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia
Kanuni ya 39 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Kamishna.
Mechi namba 58 (Yanga 1 v Simba 1). Klabu
ya Yanga imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na
mashabiki wake kurusha uwanjani chupa zinazosadikiwa kuwa na mikojo.
Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 42(1) kuhusu Udhibiti wa
Klabu.
No comments:
Post a Comment