Professor Jay amedai kuwa wasanii wa Nigeria kwa kiasi kikubwa
wamewatawala wasanii wa Tanzania na wanawapeleka vyovyote watakavyo.
Akiongea na kipindi cha XXL cha Clouds FM hivi karibuni, Professor
alisema wasanii wengi wa Tanzania wamekosa ubunifu wao wenyewe na
wamekuwa wakiiga mambo mengi kutoka Nigeria. “Hakuna mtu anakuja na idea
ya kufanya kitu tofauti, ukija na idea moja tu ikaonekana imefanya
vizuri watu wote wanahamia huko,” alisema Professor.
Professor alidai muziki wa Nigeria hauna miaka mingi ukilinganisha na ule wa Tanzania lakini hivi sasa umefika mbali kiasi cha kuutawala muziki wa Afrika.
“Najisikia aibu kusikia nipo zaidi ya miaka 20 kwenye game halafu bado napiga mark time ni jinsi gani nitakamata hata soko la Rwanda tu, ni aibu.” Alisema.
Hii ni aibu kubwa sana kwa mziki wetu, kinachotakiwa ni kufanya mziki wa Tanzania uende International kama watu wa Nigeria wanafanya kwao, na hii haiji hivihivi bali kwa kupeana support ya kutosha.
![]() |
PROFESSOR J. |
Professor alidai muziki wa Nigeria hauna miaka mingi ukilinganisha na ule wa Tanzania lakini hivi sasa umefika mbali kiasi cha kuutawala muziki wa Afrika.
“Najisikia aibu kusikia nipo zaidi ya miaka 20 kwenye game halafu bado napiga mark time ni jinsi gani nitakamata hata soko la Rwanda tu, ni aibu.” Alisema.
Hii ni aibu kubwa sana kwa mziki wetu, kinachotakiwa ni kufanya mziki wa Tanzania uende International kama watu wa Nigeria wanafanya kwao, na hii haiji hivihivi bali kwa kupeana support ya kutosha.
No comments:
Post a Comment