Thursday, May 26, 2016

KESI YA CHRISS BROWN KUHUSU MTOTO WAKE ROYALTY..

 


Kesi iliyokuwa inamkabili  staa kutoka  Marekani Chriss Brown juu ya malezi mabovu ya mtoto wake ambayo ilifunguliwa na mzazi mwenzake Nia Guzman, May 24 maamuzi yalitolewa na Mahakama ya Califonia. 

 cbbbb

Mama mtoto wa Royalty alidai kuwa Chris hana malezi sahihi na muongozo unaostahili juu ya mtoto wao, amesema Chris amekuwa akivuta sigara na bangi yeye na marafiki zake mbele ya mtoto wao na imempelekea Royalty kupata maradhi ya pumu.

Nia Guzman aliomba mahakama impunguzie Chris muda wa malezi ya mtoto huyo na kuomba yeye ndiye achukue jukumu la usimamizi wa mtoto wao kwa kipindi hiki. Chriss Brown ameshinda kesi hiyo ambapo maamuzi ya jaji yaliruhusu malezi sawa kutoka kwa wawili hao ambapo Chriss anaruhusiwa kuspend siku 12 na mtoto wake kila mwezi bila masharti yoyote.

No comments:

Post a Comment