Monday, September 29, 2014

MWANAMZIKI SIDE BOY AFARIKI DUNIA.

Muimbaji wa muziki wa Bongo Fleva Said Salim aliyekuwa akitumia jina la kisanii la Side Boy Mnyamwezi amefariki dunia.

1454892_625188920874661_1822191609_n
MAREHEMU SIDE BOY.
Side Boy amefariki jana katika hospitali ya Nyangao iliyopo mkoani Lindi. Aliwahi kutoa nyimbo kadhaa zikiwemo ‘Hujafa Hujaumbika’, ‘Usidharau Usiyemjua’ na ‘Kua Uyaone.’
Side boy alianza muziki miaka ya 2000 huku akiwa anafanya muziki tofauti na wanamuziki wengine, target ya muziki wake ilikua ni kuelimisha jamii na hata ukiona au kuskiliza tungo zake nyingi ziko katika mfumo huo, alikua mwanamuziki tofauti sana na kafanya mengi sana katika muziki wetu wa kitanzania na Mungu amlaze mahali pema peponi, Amen.

No comments:

Post a Comment